Sikiliza Tone

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

www.missdemocrasiatz.com

www.missdemocrasiatz.com

TAN

TAN

DKT

DKT

Wednesday, 28 January 2015

Wananchi watakiwa kujiepusha na vitendo vya kihalifu ili kuepusha uvunjifu wa amani nchini.

 
Na Abdulla Ali Maelezo-Zanzibar .

                                          
Wananchi wametakiwa kujiepusha na vitendo vya kihalifu ili kuepusha uvunjifu wa amani nchini. 

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mhe. Mohamed Aboud Mohamed katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani Wilaya ya Magharibi Unguja wakati akijibu swali la mwakilishi wa Jimbo la Mtambwe Mhe. Salim Abdalla Hamad.

Amesema endapo mtu atatuhumiwa kutenda vitendo hivyo vya kihalifu sheria zitatumika bila ya kumuonea au kumkandamiza mtu yeyote ili kuhakikisha amani na utulivu inabakia na kudumishwa nchini.

Amefafanua kuwa ni utaratibu wa kisheria katika nchi za Jumuiya ya Madola kwamba nchi ina mamlaka ya kumfikisha muhalifu mahakamani na kumshitaki iwapo tukio husika la kihalifu limetokea katika nchi hiyo, hivyo endapo tukio la uhalifu limetokea Tanzania Bara na endapo limetokea Zanzibar, mahakama za Zanzibar pia zinaweza kuwashitaki watuhumiwa hao.
Ametanabahisha kuwa Katiba ya Zanzibar ya 1984, kifungu cha 101 kinaweka masharti ya kikatiba ya utaratibu wa utekelezaji wa hati za mahakama ndani ya Zanzibar na Tanzania Bara kwa ujumla na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 124 imeweka masharti kama yaliyomo kwenye kifungu cha 101 cha Katiba ya Zanzibar.

No comments:

Post a Comment