Na
Abdulla Ali Maelezo-Zanzibar .
Wananchi
wametakiwa kujiepusha na vitendo vya kihalifu ili kuepusha uvunjifu wa amani
nchini.
Hayo
yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mhe. Mohamed
Aboud Mohamed katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani Wilaya ya
Magharibi Unguja wakati akijibu swali la mwakilishi wa Jimbo la Mtambwe Mhe.
Salim Abdalla Hamad.
Amesema
endapo mtu atatuhumiwa kutenda vitendo hivyo vya kihalifu sheria zitatumika
bila ya kumuonea au kumkandamiza mtu yeyote ili kuhakikisha amani na utulivu
inabakia na kudumishwa nchini.
Amefafanua
kuwa ni utaratibu wa kisheria katika nchi za Jumuiya ya Madola kwamba nchi ina
mamlaka ya kumfikisha muhalifu mahakamani na kumshitaki iwapo tukio husika la
kihalifu limetokea katika nchi hiyo, hivyo endapo tukio la uhalifu limetokea
Tanzania Bara na endapo limetokea Zanzibar, mahakama za Zanzibar pia zinaweza
kuwashitaki watuhumiwa hao.
Ametanabahisha
kuwa Katiba ya Zanzibar ya 1984, kifungu cha 101 kinaweka masharti ya kikatiba
ya utaratibu wa utekelezaji wa hati za mahakama ndani ya Zanzibar na Tanzania Bara
kwa ujumla na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 124 imeweka
masharti kama yaliyomo kwenye kifungu cha 101 cha Katiba ya Zanzibar.
No comments:
Post a Comment